Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks
Home » , » POGBA APEWA NAMBA MPYA

POGBA APEWA NAMBA MPYA

paul-pogba
Nchini Italia kiungo ambaye amekuwa gumzo kwenye soko la usajili akitajwa kuwa mbioni kujiunga na karibu timu zote kubwa Paul Pogba amekabidhiwa jezi namba 10 ambayo atakuwa akiivaa kwa msimu ujao katika michuano mbalimbali ya ndani nan je .
Pogba mwenye umri wa miaka 22 anakabidhiwa jezi namba 10 baada ya mshambuliaji Carlos Tevez ambaye alikuwa anavaa jezi hiyo kuhamia Boca Juniors hali iliyofungua fursa ya jezi hiyo kukabidhiwa kwa Pogba.
Pogba anakuwa Mfaransa wa pili kuvaa jezi namba 10 kwenye klabu ya Juventus baada ya gwiji mwingine Michel Platini ambaye kwa sasa ni rais wa UEFA kuvaa jezi namba 10 katika miaka ya 80 wakati akiwa anaicheza klabu hii .
Ukiachilia mbali kuondoka kwa Tevez kuacha jezi namba 10 kuwa wazi, wadadisi wa mambo wanaamini kuwa huenda hii ikawa mbinu ya kumvutia mchezaji uyo kumfanya endelee kubaki na Juventus hasa ukizingatia kuwa amepokea ofa nyingi zinazomtaka kuihama klabu hiyo.
Blog inayotoa habari kila siku Karibu Ungana na Mwandishi wetu kila siku hapa Jafar Nzowa

0 maoni:

Chapisha Maoni

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. JAFAR NZOWA JR - All Rights Reserved
Template Modify by Creating Website
Proudly powered by Blogger