Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks
Home » , » BARUA YA WAZI YA DI MARIA KWA MASHABIKI WA MANCHESTER UNITED

BARUA YA WAZI YA DI MARIA KWA MASHABIKI WA MANCHESTER UNITED

 
Baada ya kujiunga na PSG kwa dau la paundi milioni 44, winga wa kimataifa wa Argentina,
Angel di Maria amewaandikia barua ya wazi mashabiki wa klabu ya Manchester United ambayo ameichezea kwa mwaka mmoja.
Di Maria alisajiliwa na Man United kutokea Real Madrid kwa ada ya paundi milioni 60 na kuvunja rekodi ya usajili ya soka la England.
BARUA YA WAZI YA ANGEL DI MARIA KWA MASHABIKI WA MANCHESTER UNITED
"Naandika barua hii kuishukuru familia nzima ya Manchester United kwa kuniunga mkono kwa mwaka mmoja niliokuwa sehemu ya klabu.
Manchester United waliponichagua kuwa sehemu ya timu yao, nilijisikia kuheshimiwa kwasababu nilijua klabu hii ina maanisha nini na jinsi gani iliniamini.
Hata hivyo, nafahamu mambo hayakwenda vizuri kama tulivyotarajia, naomba msamaha kwa hilo.
Katika maisha ya mcheza mpira, kuna wakati mwingine mambo usiyotarajia na usiyoyataka yanatokea.
Nawahakikishia kwamba haikuwa kujaribu. Nilijitahidi niwezavyo, lakini mpira sio kama hesabu: Mara zote kuna vitu vingi vinavyoathiri vile unavyofikiria.
Samahani sana kwasababu sikufanya kile nilichotarajia katika klabu hii kubwa na ya ajabu.
Natoa shukurani za pekee kwa bodi ya wakurugenzi na utawala ya Manchester United, vilevile kila kiongozi na wachezaji wenzangu walioniunga mkono.
Pia shukurani za pekee ziwaendee mashabiki ambao mara zote waliniamini na kuonesha heshima na mapenzi makubwa.
Sasa ni wakati wa kujiunga na PSG, lakini Utukufu wa Manchester United utabaki kwenye kumbukumbu zangu daima.
Nawatakia kila la kheri
Angel di Maria".
Blog inayotoa habari kila siku Karibu Ungana na Mwandishi wetu kila siku hapa Jafar Nzowa

0 maoni:

Chapisha Maoni

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. JAFAR NZOWA JR - All Rights Reserved
Template Modify by Creating Website
Proudly powered by Blogger