Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks
Home » » MESSI NA NEYMAR WAWAKERA MASHABIKI

MESSI NA NEYMAR WAWAKERA MASHABIKI


Mashabiki wa Barcelona wa America kaskazini wame-maindi kinoma baada ya kugundua kwamba nyota wakubwa wa klabu hiyo hawamo katika ziara ya Marekani itayoanza wiki ijayo.

Barcelona wametaja kikosi cha wanandinga 24 wataokwenda ziara ya Marekani itayoanza Julai 19-29 mwaka huu, lakini nyota wake wawili, Lionel Messi na Neymar wameachwa kwasababu kocha mkuu, Luis Enrique amewaongezea siku katika likizo yao.

Messi na Neymar walishiriki  michuano ya Copa America iliyomalizika siku za karibuni kwa Chile kuibuka Machampion.
Lakini sio wao tu, wachezaji wote waliocheza Copa America kama vile Claudio Bravo, Javi Mascherano na Dani Alves  pia wameondolewa katika ziara hiyo ya Marekani.

HIKI NDICHO KIKOSI CHA BARCELONA CHA WACHEZAJI 24 WANAOKWENDA ZIARA YA MAREKANI


Ter Stegen, Masip, José Suárez, Piqué, Rakitic, Sergio, Pedro, Iniesta, Suárez, Rafinha, Bartra, Douglas, Jordi Alba, S. Roberto, Adriano, Vermaelen, Mathieu, Arda Turan, Aleix Vidal, Sandro, Munir, Halilovic, Samper, Gumbau
Blog inayotoa habari kila siku Karibu Ungana na Mwandishi wetu kila siku hapa Jafar Nzowa

0 maoni:

Chapisha Maoni

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. JAFAR NZOWA JR - All Rights Reserved
Template Modify by Creating Website
Proudly powered by Blogger