Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

LEO NDIO LEO MAPINDUZI CUP

SIMBA VS AZAM

ANGALIA PICHA ZA MAPOKEZI YA DIAMOND PLATNUMZ JANA

Photos: Mapokezi ya Diamond Platnumz na Tuzo
Screenshot_2015-10-16-00-09-47_1 Screenshot_2015-10-16-00-09-56_1 Screenshot_2015-10-16-00-10-01_1 Screenshot_2015-10-16-00-10-06_1 Screenshot_2015-10-16-00-10-11_1 Screenshot_2015-10-16-00-21-03_1 Screenshot_2015-10-16-00-21-14_1

MAGUFULI NA MAFURIKO CHATO PAMOJA NA WASANII KIBAO

Kundi la Orijino Komedi likikamua jukwaani.

 Maelfu wa wakazi wa Chato wakisikiliza kwa makini sera za Mgombea Urais kupitia CCM, John Magufuli.
 
Wakazi wa Chato wakionesha mabango yao mbalimbali.

Nyomi ya wanachama wa CCM kama inavyoonekana leo hii huko Chato.

Msanii wa Bongo Fleva, Madee akitoa burudani kwa wakazi wa Chato.

Kundi la Yamoto Band wakikamua jukwaani, katikati ni densa wa Yamoto, Chiba.

Staa wa Hip Hop, Fid Q akitoa burudani.

Magufuli akiwafunika Chegge na Temba.

Kundi la Orijino Komedi likikamua jukwaani.

Mgombea Urais kupitia CCM, John Magufuli akiingia Viwanja vya Chato
Mgombea Urais kupitia CCM, John Mafuguli leo alifanya mkutano mkubwa wa kuomba kura katika Viwanja vya Chato ambapo ndipo nyumbani kwake. Mkutano huo ulihudhuriwa na umati mkubwa wa watu.
Katika mkutano huo wasanii mbalimbali walitoa buurudani ambapo walipopanda wasanii wa kundi la TMK Wanaume familiy Chegge na Temba Magufuli alishindwa kujizuia na kuanza kusakata nao jukwaani na kuwafunika wasanii hao hali iliyozua shangwe kubwa kwenye viwanja hivyo.
Sambamba na burudani hiyo Magufuli alimwaga sera na kutoa ufafanuzi wa jinsi atakavyoikwamua Tanzania kutoka katika lindi la umasikini mijini na vijijni.

Mabango 5 Bora Katika Siasa Leo.

WANA CCM WAHAMIA ACT


Zaidi ya wanachama 100 kutoka CCM, Kata ya Chihanga, Manispaa ya Dodoma wamejiunga na ACT- Wazalendo.

Akizungumza kwa niaba ya wanachama hao, Ally Amanzi aliyekuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa CCM katika kata hiyo, alisema jana kuwa wamelazimika kuhama kutokana na kufilisika kisiasa.

Amanzi alisema viongozi wa vyama hawaonyeshi kama wanaweza kuleta mabadiliko, badala yake wanafikiria watakavyojilimbikizia mali.

“ACT–Wazalendo tunaimani nayo sisi wakazi wa Kata ya Chihanga, lazima tutapata mabadiliko ya kweli tofauti na vyama vingine vinavyojitokeza kuomba viongozi wao tuwachague,” alisema Amanzi. 
 
Alisema katika chama hicho kuna ubabaishaji mwingi, hali inayochangia wananchi wasipate maendeleo.

Walence Lusingu ambaye aliwahi kuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM, Mkoa wa Dodoma, alisema ACT kimedhamiria kuwaletea maendeleo ya kweli wananchi wa kata hiyo.

Lusingu ambaye ni mgombea udiwani katika Kata ya Miyuji, aliwataka wakazi wa kata hiyo kutofanya makosa ya kuchagua viongozi wa vyama vya siasa ambavyo vitawageuza kuwa mitaji pindi vitakapochaguliwa kushika madaraka. 
 
Alisema katika kipindi hiki cha kampeni, lazima wawe makini katika kusikiliza sera zinazotolewa na wagombea hao, kutokana na wengi wamekuwa wakijinadi kwa kutoa maneno matamu huku wakiwa siyo wakweli.

Mgombea udiwani wa Kata ya Chihanga ambaye alikuwa diwani kupitia CCM kabla ya kuhamia ACT- Wazalendo, Julia Mputu amewaomba wananchi wa kata hiyo, kumpa ridhaa tena ya kumrudisha madarakani ili amalize miradi iliyobaki wakati wa kipindi chake.

Mputu alisema katika kipindi chake cha udiwani, mahitaji ambayo walikuwa wamemtuma mengi ameyafanikisha na machache hajakamilisha.

Aliyataja baadhi ya mambo aliyofanikisha kuwa ni barabara, afya, elimu pamoja na suala ya kilimo.

Hata hivyo, alisema miradi iliyobaki ataikamilisha watakapomchagua katika uchaguzi utakaofanyika mwezi ujao.

“Nawaomba mnirudishe nije tumalizie miradi iliyobaki ukizingatia kuwa kazi yangu niliyoifanya kwa kushirikiana na ninyi mmeiona kwa vitendo. Hakukuwa na ubabaishaji wowote,” alisisitiza.

Hiki ndio kikosi cha Simba msimu 2015/2016


Hiki ndio kikosi cha Simba msimu 2015/2016

Klabu ya Simba imekamilisha usajili ramsi na hiki ndio kikosi chake kitakachoshiriki katika msimu mpya wa ligi kuu ya Vodacom 2015/2016.
Hii ndio orodha ya wachezaji wote wa Simba waliosajiliwa msimu wa 2015/2016
  1. Vincent De Paul Angban
  2. Peter Manyika
  3. Denis Deonis
  4. Mohamed Hussein
  5. Hassan Ramadhani
  6. Emery Nimubona
  7. Samih Ali Nuhu
  8. Hassan Isihaka
  9. Murushid Juuko
  10. Mohamed Faki
  11. Saidi Issa
  12. Abdi Banda
  13. Jonas Mkude
  14. Justice Majabvi
  15. Awadh Juma
  16. Saidi Hamisi Ndemla
  17. Mwinyi Kazimoto
  18. Peter Mwalyanzi
  19. Hajibu Ibrahim
  20. Issa Abdallah
  21. Daniel Lyanga
  22. Hamisi Kizza
  23. Pape Abdoulaye Ndaw
  24. Mussa Hasan Mgosi
  25. Boniphace Maganga
  26. Simon Serunkuma
  27. Joseph Kimwaga

TIMU ZA VPL NA JEZI ZAO MSIMU HUU

002.SPORT
Kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania, ambayo ni mdhamini mkuu wa Ligi Kuu ya mpira wa miguu Tanzania bara leo imekabbidhi vifaa kwa timu zinazoshiriki ligi hiyo yenye thamani ya shilingi milioni 490,00,000.

Akikabidhi vifaa hivyo leo jijini Dar es salaam, Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Kelvin Twisa alsiema kuwa kwa mara nyingine tena katika kuhakikisha ligi ya soka nchini inaenda vizuri Vodacom inakidhi vifaa mbalimbali vy a ligi ambavyo ni jezi za kawaida, jezi za mechi, viatu na vifaa vingine vinayohitajika.

“Tunajisikia furaha kukabidhi vifaa hivi siku ya leo tukiwaa tunatekeleza matakwa ya mkataba wa udhamini, ni imani yetu kwamba timu zitakazoshiriki lii zimejiandaa vya kutosha kwa msimu mpya 2015/2016” Alisema Twissa.

Twissa alisema Vodacom inaendelea kudhamini ligi kuu kwa sababu soka ni mchezo unaopendwa sana hapa nyumbani ukiwa na washabiki wengi hivyo inapenda kuona wananchi ambao baadhi yao ni wateja wake wanapata buruddaniya mchezo waupendao pia siku zote inaamini kuwa michezo ni ajira kubwa duniani kote, ikiendelezwa inaweza kubadilisha maisha ya watu wengi na taifa kunufaika kwa mapato makubwa ya kodi kutoka sekta hii.

Aliwataka wadhamini wengine kujitokeza ili kuboresha zaidi ligi ya Tanzania na kuongeza maslahi kwa wachezaji wanaoshiri katika ligi “Tukiunganisha nguvu timu zetu zinaweza kuwa na wachezaji wa kimataifa pia ni muhimu kwa wadau mbalimbali kuanza kuwekeza katika timu za vijana chipukizi kwa kuwa vipaji vinaanza ngazi ya chini ambako vinapaswa kuibuliwa na kuendelezwa” Alisema Twissa.
003.SPORT-AFRICAN%2BSPORT%2BTANGA
Wawakilishi wa kionyesha jezi za Mtibwa Sugar, (picha na michuzi blog)
Naye Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi, Boniface Wambura aliishukuru Kampuni ya Vodacom na kuvitaka vilabu vinavyoshiriki ligi kuu ya Vodacom kuheshimu chapa ya mdhamini wakati wote wa ligi.

“Ninatoa mwito kwa vilabu vyote kutumia jezi zenye nembo ya mdhamini katika kuhakikisha ligi inafanikiwa kama inavyotakiwa” alisema.

Aliongeza kuwa TFF isingependa kutumia kanuni na sharia kuadhibu klabu inayokwenda kinyume, bali kila klabu izingatie masharti ya madhamini kama ambavyo anavyotimiza haki yake ya kuwapatia vifaa.

Alisema ligi ya mwaka huu itakuwa bora kutokana na maandalizi yote kukamilika mapema pia timu zitakazoshiriki zimejiandaa vya kutosha kuhakikisha ligi inakuwa na msisimko na ushindani mkubwa.


004.MAJIMAJI
Wawakilishi wa Kagera Sugar wakionyesha jezi za nyumbani na ugenini za timu hiyo (picha na michuzi blog)
006.COASTA%2BUNION
Wakionyesha jezi za Coastal union za nyumbani na ugenini (picha na michuzi blog)
007.MBEYA%2BCITY
Jezi za Mbeya City nyumbani na ugenini (picha na michuzi blog)
008.YANGA
Jezi za Yanga nyumbani na ugenini (picha na michuzi blog)
010.SIMBA
Jezi za Simba SC za nyumbani na ugenini (picha na michuzi blog)
CN6PzllWEAAgVYf
Jezi za Stand United za ugenini na nyumbani
009.SPORT
Picha ya Pamoja katika utoaji wa vifaa vya michezo kwa vilabu
 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. JAFAR NZOWA JR - All Rights Reserved
Template Modify by Creating Website
Proudly powered by Blogger