Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks
Home » » TAMBWE NA BUSUNGU WAWAPIGISHA GWARIDE ASKARI JELA

TAMBWE NA BUSUNGU WAWAPIGISHA GWARIDE ASKARI JELA

 
Mabingwa wa kandanda Tanzania bara, Young Africans wameinyuka Tanzania Prisons 2-0 katika mechi ya kirafiki iliyopigwa uwanja wa Sokoine, jijini Mbeya.
Magoli ya Yanga yamefungwa na washambuliaji wake hatari, Malimi Busungu na Amissi Tambwe kwa kila kipindi.
Donald Ngoma na Geofrey Mwashiuya walijitahidi kucheza kwa kiwango kizuri, lakini walishindwa kucheka na nyavu.
Kiujumla Yanga imetandaza soka murua katika mchezo huo uliokuwa  wa kujipima nguvu kwa makocha wote wawili, Salum Mayanga (Tanzania Prisons) na Hans van der Pluijm (Yanga).
Nao Prisons walijitahidi kushambulia mara kadhaa, lakini ngome ya Yanga ilikuwa imara.
Mbali na hayo, mechi hiyo ilitawaliwa na ubabe wa hapa na pale ambapo Mwinyi Hajji alitolewa kwa kadi nyekundu.
Mwashiuya aliifungia Yanga mabao mawili katika ushindi wa 4-1 waliovuna dhidi ya Kimondo FC katika mechi ya kwanza ya kirafiki iliyopigwa mwishoni huko Vwawa Mbozi.
Mwishoni mwa Juma hili, Yanga inatarajia kushuka uwanjani tena kuchuana na Mbeya City katika uwanja huo wa Sokoine.
Kiingilio katika mechi hiyo kitakuwa shilingi  40,000/.
Blog inayotoa habari kila siku Karibu Ungana na Mwandishi wetu kila siku hapa Jafar Nzowa

0 maoni:

Chapisha Maoni

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. JAFAR NZOWA JR - All Rights Reserved
Template Modify by Creating Website
Proudly powered by Blogger