Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks
Home » » AKINA NGASA WAFUMULIWA NA AKINA TSHABALALA

AKINA NGASA WAFUMULIWA NA AKINA TSHABALALA

Siphiwe Tshabalala alipigia msumari wa moto jeneza la Free State jana 

TIMU ya Free State Stars yenye Mtanzania, Mrisho Khalfan Ngassa imefungwa mabao 4-0 jana na Kaizer Chiefs katika mchezo wa Ligi Kuu ya ABSA Afrika Kusini Uwanja wa FNB, Johannesburg.
Huo unakuwa mchezo wa pili Free State kufungwa, baada ya wiki mbili zilizopita kufungwa 1-0 nyumbani na Mpumalanga Blac Aces. 
Katika mchezo wa jana ambao Ngassa hakucheza, mabao ya Kaizer Chiefs yalifungwa na Siboniso Gaxa dakika ya 34, George Lebese dakika ya 42, Chakoroma Liberty aliyejifunga dakika ya 45 na Siphiwe Tshabalala dakika ya 66.
Kikosi cha Kaizer Chiefs kilikuwa: Khune, Gaxa, Mathoho, Xulu, Masilela, Tshabalala, Letsholonyane, Katsande, Lebese/Maluleka dk73, Parker/Karuru dk80, Mthembu/Ndulula dk66.
Free State Stars: Mathole, Mashego, Chakoroma, Sankara, Thlone, Venter/Somaeb dk54, Kerspuy, Masehe, Obada/Thetani dk54, Ngcobo/Fileccia dk69 na Mohomi.
Blog inayotoa habari kila siku Karibu Ungana na Mwandishi wetu kila siku hapa Jafar Nzowa

0 maoni:

Chapisha Maoni

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. JAFAR NZOWA JR - All Rights Reserved
Template Modify by Creating Website
Proudly powered by Blogger