Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks
Home » , » MBOWE ASEMA YUPO SALAMA

MBOWE ASEMA YUPO SALAMA

 Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe.

Mwanasheria mkuu wa Chadema Tundu  ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki, amesema kuwa Mwenyekiti wake Freeman  Mbowe yuko salama na anaendelea vizuri.
Licha Tundu Lissu kusisitiza kuwa Mwenyekiti wake yuko vizuri, Mwenyekiti huyo  amezungumza na Waandishi wa Habari leo ambapo amesema afya yake imeimarika na anendelea vizuri.
Aidha, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe jana aliugua ghafla akiwa katika maandamano ya kumsindikiza mgombea urais kwa tiketi ya chama hicho, Edward Lowassa baada ya kuchukua fomu za kugombea urais katika Tume ya Taifa Uchaguzi (NEC).
Katika msafara huo  wakiwa njiani Mbowe na Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu walikuwa wamechomoza kwenye gari wakiwapungia wananchi waliojitokeza kwenye maandamano  hayo lakini baadae  hali yake ilibadilika na kukimbizwa hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam.
Blog inayotoa habari kila siku Karibu Ungana na Mwandishi wetu kila siku hapa Jafar Nzowa

0 maoni:

Chapisha Maoni

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. JAFAR NZOWA JR - All Rights Reserved
Template Modify by Creating Website
Proudly powered by Blogger