Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks
Home » » MAJIMBO MATANO YA CCM KURUDIA UCHAGUZI

MAJIMBO MATANO YA CCM KURUDIA UCHAGUZI

https://24tanzania.com/wp-content/uploads/2013/04/75f2Nape-Nnauye.jpg
Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM,Nape Nnauye.

Kamati kuu ya chama cha Mapinduzi imeyataka majimbo matano nchini Tanzania kurudia mchakato wa kura za maoni ambao ulimalizika wiki iliyopita  huku baadhi ya maeneo matokeo yakipingwa vikali.
Akizungumza na Mwandishi wa Mtandao wa Hivisasa nje ya makao makuu ya CCM mkoani Dodoma  katibu wa Itiakadi na Uenezi Nape Nnauye amesema kutokana  na kasoro zilizojitokeza kamati kuu imeagiza majimbo matano  yarudie kura za maoni na zoezi hilo lifanyike  kesho kutwa siku ya alhamisi tarehe 13,8,2015 na matokeo yake yataletwa kwa ajili ya uamuzi.
Nape ameyataja majimbo hayo  kuwa   ni Rufiji, Kilolo, Makete, Busega  na  Ukonga.
Matokeo katika baadhi ya majimbo hayo ni,
JIMBO LA  MAKETE
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Dk. Binillith Mahenge, ametetea nafasi yake katika jimbo la Makete baada ya kuibuka mshindi mwembamba.
JIMBO LA UKONGA
Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Slaa amepata ushindi wa kura 10,000 dhidi ya Raesh Patel kura 7,356 na Rober Masegesi kura 548.
“Majimbo hayo matano yatarudia uchaguzi wa kura za maoni kutokana na kasoro mbalimbali zilizojitokeza wakati wa zoezi hilo” Amesema Nape
Katika Hatua nyingine Nape amesema vikao  vya Kamati ya Maadili na Kamati kuu ya CCM vina endelea  katika ukumbi wa White House Makao Makuu Dodoma chini ya Mwenyekiti wa Chama hicho Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.
Blog inayotoa habari kila siku Karibu Ungana na Mwandishi wetu kila siku hapa Jafar Nzowa

0 maoni:

Chapisha Maoni

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. JAFAR NZOWA JR - All Rights Reserved
Template Modify by Creating Website
Proudly powered by Blogger