Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks
Home » » WABAGUZI WAFUNGIWA MIAKA MITANO

WABAGUZI WAFUNGIWA MIAKA MITANO

Mashabiki wanne wa kilabu ya Chelsea walioshtumiwa kwa kukataa kumruhusu mtu mmoja mweusi kuingia katika treni ya Paris Metro mashabiki hao  wamepigwa marufuku kuhudhuria mechi za soka kwa takriban miaka mitano.
 
Richard Barklie,kutoka Carrickfergus,Northern Ireland na Joshua Parsons pamoja na William Simpson wote kutoka Surrey walipigwa marufuku kwa miaka mitano katika mahakama ya Stratford.
Jordan Munday ,kutoka eneo la Sidcup Kent,alipigwa marufuku ya miaka mitatu.

Waliagizwa kwamba hawawezi kuhudhuria mechi nyumbani ama ugenini.
Jaji wa wilaya Gareth Branston alisema kwamba chuki ya kibaguzi zilionyeshwa na mashabiki wa Chelsea katika treni hiyo ya Paris.

Aliaambia mahakama hiyo kwamba kisa hicho kiliharibu sifa ya soka ya Uingereza barani Ulaya.

Ghasia zilizuka wakati mashabiki wa Chelsea walipokuwa katika mji huo wa Ufaransa ili kushabikia mechi ya vilabu bingwa Ulaya kati ya Chelsea na Pasris Saint Germain tarehe 17 februari.

Baadaye kanda ya video iliibuka ikimuonyesha raia mmoja wa Ufaransa Souleymane Sylla akisukumwa nje ya treni.

Blog inayotoa habari kila siku Karibu Ungana na Mwandishi wetu kila siku hapa Jafar Nzowa

0 maoni:

Chapisha Maoni

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. JAFAR NZOWA JR - All Rights Reserved
Template Modify by Creating Website
Proudly powered by Blogger