Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks
Home » » MTOTO WA MIAKA 15 ASHIKILIWA KWA UJAMBAZI KITUO CHA STAKISHARI

MTOTO WA MIAKA 15 ASHIKILIWA KWA UJAMBAZI KITUO CHA STAKISHARI

Jeshi la Polisi kanda Maalum ya Dar es salaam inawashikilia watu wawili akiwemo mtoto wa miaka 15 kwa kujihusisha na matukio mbalimbali ya ujambazi likiwemo tukio la uvamizi na mauaji kituo cha Polisi Stakishari.

Mbali na hilo jeshi hilo limefanikiwa kukamata bunduki 16 kati ya hizo 14 ziliibiwa katika tukio la stakishari, ambazo zilikuwa chini ya handaki Wilaya ya Mkuranga pamoja na milioni 170.
Suleiman Kova alisema watuhumiwa hao pamoja vitu hivyo vilikamatwa kutokana na msako wa unaoendelea wa kupambana na makosa mbalimbali ya uhalifu kwa kutumia silaha za moto.
“Julai 17 zilipatikana taarifa za eneo la Taungoma kulikua na majambazi waliohusika kwenye tukio la stakishari, wakijiandaa kufanya tikio la uhalifu, kikosi kilikwenda haraka eneo la tukio na kuweka mtego na kufanikiwa kuwanasa washukiwa watano…walainza kupambana  baada ya kukataa kusimama na majambazi watatu walifariki dunia”Kova.
Alisema silaha 14 zilizopatikana  ziliporwa katika kituo cha stakishari bado hazijakamilisha idadi ya zilizopotea na jeshi hilo bado linaendelea na msako.
Kova alisema ndani ya shimo pia wlaikuta silaha ya kichina aina ya Norinko ambayo haitumiwi na majeshi ya Tanzania, risasi 25 pamoja na fedha taslimu milioni 170 ambazo zilifungwa katika sanduku maalum la kabati.
Blog inayotoa habari kila siku Karibu Ungana na Mwandishi wetu kila siku hapa Jafar Nzowa

0 maoni:

Chapisha Maoni

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. JAFAR NZOWA JR - All Rights Reserved
Template Modify by Creating Website
Proudly powered by Blogger