Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks
Home » » MORGAN SCHNEIDERLIN AANZA MAMBO MANCHESTER UNITED

MORGAN SCHNEIDERLIN AANZA MAMBO MANCHESTER UNITED

Schneiderlin akipaa juu na kupiga kichwa kilichozaa goli

Morgan Schneiderlin, Memphis Depay, Matteo Darmian na Bastian Schweinsteiger  wote wamecheza mechi yao ya kwanza Manchester United ikishinda goli 1-0 dhidi ya Club America katika mechi ya kwanza ya michuano ya International Champions Cup  iliyopigwa asubuhi hii uwanja wa Seattle, Marekani.
Schneiderlin ndiye amefunga goli pekee la ushindi dakika 5 tu ya kipindi cha kwanza akimalizia krosi  ya Juan Mata.

Mfaransa Depay na Darmian wote walitolewa na Louis van Gaal, huku Schweinsteiger akiingia kucheza mechi yake ya kwanza katika klabu hiyo.
Schweinsteiger  amecheza vizuri na kuifanya United itawale mchezo kipindi cha pili, lakini walishindwa kuongeza bao.
Blog inayotoa habari kila siku Karibu Ungana na Mwandishi wetu kila siku hapa Jafar Nzowa

0 maoni:

Chapisha Maoni

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. JAFAR NZOWA JR - All Rights Reserved
Template Modify by Creating Website
Proudly powered by Blogger