Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks
Home » , » Mbwana Samatta; Bado nina ndoto ya kucheza klabu bingwa ya dunia…..

Mbwana Samatta; Bado nina ndoto ya kucheza klabu bingwa ya dunia…..

Mshambulizi wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Samatta amesema amesalia na nafasi moja tu ya kucheza Klabu bingwa ya dunia. Akizungumza na mwandishi wa mtandao huu ( Baraka Mbolembole) Jumanne hii, Samatta ambaye amebakiza miezi 8 katika mkataba wake wa sasa.
Samatta ataachana na TP Mazembe ya DR Congo klabu ambayo alijiunga nayo Mei, 2011 akitokea Simba SC. " Nimebakiwa na nafasi moja tu, nayo ni ushiriki wa TP katika ligi ya mabingwa msimu huu ambako tuko robo fainali. Kama timu itafanya vizuri, naweza kucheza michuano ya Klabu bingwa ya dunia"
Samatta amedhamiria kuachana na TP ambayo tangu amejiunga nayo ameshuhudia wachezaji wasiozidi saba wakiuzwa nje au ndani ya bara la Afrika. Mazembe tayari imecheza michezo miwili katika hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa lakini haijapata ushindi wowote na wamecheza mechi zote hizo pasipo kufunga goli lolote.
" Nimeshiriki karibu dakika 120 katika michezo miwili ambayo tumecheza katika nane bora. Suala la kupata goli/magoli ni kutokana na upinzani tunaokutana nao. Kitu kizuri pia, hatujaruhusu goli. Kwa hiyo unaweza kuona upinzani jinsi ulivyo" anasema Samatta na kuongeza
 " Tangu nimejiunga hapa ni wachezaji wasiozidi Saba wameuzwa. Ukweli sijafanya mawasiliano na mchezaji yeyote ambaye alikuwa akichezea TP. Nahitaji changamoto mpya. Wakala wangu bado anashughurika na hilo. Dirisha la usajili liko wazi hivyo lolote linaweza kutokea "
Habari za ndani ambazo pia ninazo ni kwamba, mchezaji huyo wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars anaweza kuwa mchezaji anayelipwa zaidi barani Afrika kama hatokwenda barani ulaya mara baada ya kumalizika mkataba wake wa sasa. Samatta aliondoka Tanzania akiwa na miaka 19. " Nafasi ya kusaini mkataba mpya hapa ni ndogo sana" anamaliza kusema mchezaji huyo mwenye miaka 23 hivi sasa
Blog inayotoa habari kila siku Karibu Ungana na Mwandishi wetu kila siku hapa Jafar Nzowa

0 maoni:

Chapisha Maoni

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. JAFAR NZOWA JR - All Rights Reserved
Template Modify by Creating Website
Proudly powered by Blogger