Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks
Home » » MAREKANI YAUA WANAJESHI WA AFGHANSTAN

MAREKANI YAUA WANAJESHI WA AFGHANSTAN

Shambulizi la anga la Marekani lasababisha vifo vya wanajeshi 8 wa Afghanistan 
 
Takriban askari wanane wa Afghanistan wamekufa katika shambulio la anga la Marekani kwenye kituo cha kijeshi cha ukaguzi katika jimbo la Logar kusini mwa mji mkuu Kabul, kwa mujibu wa maafisa wa Afghanistan.
Wanasema helikopta za Marekani zilishambulia kituo hicho cha ukaguzi wakati wa mchana Jumatatu.
Wanajeshi kadhaa wamejeruhiwa.
Kamanda wa jeshi katika eneo hilo ameiambia BBC kuwa kituo hicho cha ukaguzi kilikua kinapeperusha wazi bendera ya Afghanistan.
Hali ya usalama katika jimbo la Logar inayumba ambapo maeneo mengi ya vijijini vimo mikononi mwa wapiganaji wa Taliban.
 null
Wanajeshi kadhaa wamejeruhiwa.
Mwandishi wa BBC David Loyn aliyeko mjini Kabul anasema kuna mkanganyiko mkubwa kuhusu tukio la leo asubuhi katika wilaya ya Baraki Barak .
Mwandishi wetu anasema juhudi za uokozi zinatatizwa na makundi ya waasi wanaowashambulia kwa risasi wanajeshi wa Afghanstan.
Msemaji wa vikosi vya kimataifa nchini humo anasema wanafahamu kuhusu tukio hilo linalovihusisha vikosi vya Marekani na kwamba wanalifanyia uchunguzi.


Chanzo: BBC
Blog inayotoa habari kila siku Karibu Ungana na Mwandishi wetu kila siku hapa Jafar Nzowa

0 maoni:

Chapisha Maoni

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. JAFAR NZOWA JR - All Rights Reserved
Template Modify by Creating Website
Proudly powered by Blogger