Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks
Home » , » KIBURI KUMTOA VALDES OLD TRAFFORD

KIBURI KUMTOA VALDES OLD TRAFFORD


 
 KLABU ya Manchester United iko tayari kumuuza Victor Valdes baada ya Louis van Gaal kukerwa na kitendo cha kipa huyo kugoma kuchezea kikosi cha pili msimu uliopita.

Mlinda mlango huyo mwenye umri wa miaka 33 ameachwa kwenye msafara wa United uliokwenda ziara ya Marekani na anaendelea kufanya programu maalumu ya kumuweka fiti viwanja vya Carrington chini ya Mtaalamu wa maungo.

Valencia na klabu za Uturuki ni miongoni wanaomtaka kipa huyo, wakat United inamtaka mchezaji huru, Sergio Romero azibe pengo lake.

Mashabiki wa Manchester United walistaajabishwa na jina la Valdes kutokuwemo kwenye kikosi cha Louis van Gaal kilicjokwenda ziara ya kujiandaa na msimu.

"Valdes hajateuliwa (katika ziara) kwa sababu hafuati falsafa zangu. Falsafa ni jinsi gani unacheza soka na jinsi gani unalinda ladha ya uchezaji wako,"amesema Van Gaal.

"Aligoma msimu uliopita kuchezea timu ya pili. Kuna mengi katika upande mwingine wa falsafa, namna gani unatakiwa kucheza kama kipa Manchester United. Kama haujaridhia  [kufuata] utaratibu wa falsafa hiyo kuna njia moja tu, na hiyo ni kuondoka,"amesema Van Gaal.
Blog inayotoa habari kila siku Karibu Ungana na Mwandishi wetu kila siku hapa Jafar Nzowa

0 maoni:

Chapisha Maoni

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. JAFAR NZOWA JR - All Rights Reserved
Template Modify by Creating Website
Proudly powered by Blogger