Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks
Home » , » NYUMBA YA CHRIS BROWN YAVAMIWA

NYUMBA YA CHRIS BROWN YAVAMIWA

 
Nyumba ya nyota wa muziki Chris Brown kutoka Marekani imevamiwa na kupekuliwa na watu watatu waliofunika nyuso zao ambao walimfungia shangazi lake ndani chumba chake kulingana na maafisa wa polisi.
Nyota huyo wa muziki wa R&B hakuwepo nyumbani kwake wakati wa wizi huo ambao ulifanyika alfajiri siku ya jumatano.
Maafisa wanasema kuwa washukiwa ambao walikuwa na bunduki waliondoka katika jumba hilo la Tarzana na fedha za kiasi kisichojulikana pamoja na vitu kadhaa vya kibinafsi.
Brown au wawakilishi wake bado hawajatoa tamko lolote kuhusu tukio hilo.

Chris Brown na Rihanna kabla ya wawili hao kukosana
Kulingana na ripoti,nyota huyo alikuwa ameenda kujivinjari katika kilabu moja wakati wa kisa hicho
Hii ni mara ya pili ya nyumba ya msanii huyo ambaye alikuwa mpenziwe nyota wa muziki wa Pop Rihanna kuvamiwa katika kipindi cha miezi ya hivi karibuni.
Mnamo mwezi Mei,aliwasili nyumbani na kumpata mwanamke mmoja aliyedaiwa kuvunja na kuingia kupika vyakula kadhaa na kuandika ukutani kwamba anampenda msanii huyo.


Source: BBC
Blog inayotoa habari kila siku Karibu Ungana na Mwandishi wetu kila siku hapa Jafar Nzowa

0 maoni:

Chapisha Maoni

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. JAFAR NZOWA JR - All Rights Reserved
Template Modify by Creating Website
Proudly powered by Blogger